Saturday, October 19, 2013

MAAJABU YA MWILI WA BINADAMU

1.Joto linalozalishwa na mwili wa binadamu kwa muda wa nusu saa linatosha kufanya nusu galoni la maji lichemke! Hii inamaanisha kwamba joto la mwili linaweza kuchemsha galoni zima la maji kwa lisaa limoja.
















2.Inakadiriwa kwamba mtu wa kawaida mwenye miaka 70 huwa tayari ametengeneza galoni 6250 za MATE katika maisha yake. Kiasi hicho kinatosha kujaza mabwawa mawili ya kuogelea! (swimming pools)




















3. Mishipa iliyoko mwilini kwa mtu mzima ikiunganishwa pamoja inaweza kufikia urefu wa maili elfu sitini (60,000) au kilomita 96,560. Kwa urefu huo mishipa ya binadamu mmoja inawaza ikaizunguka dunia mara mbili, kwani mzingo wa dunia ni kilomita 40,075!
























4. Moyo wa binadamu husukuma lita 445 za damu kila siku, Hizo ni sawa na ndoo kubwa 23 za maji
























5. Tindikali inayozalishwa kwenye tumbo la binadamu ina uwezo wa kuyeyusha viwembe





6. Binadamu hawezi kupiga chafya akiwa amefungua macho

7. Kusikiliza muziki baada ya kula kunasaidia mmeng'enyo wa chakula (digestion) ufanyike kwa ufanisi zaidi


8. Kukosa usingizi kunachangia mtu kushambuliwa na magonjwa mara kwa mara. Hii ni kwa sababu usingizi ni muhimu katika kutengeneza kinga ya mwili

9. Kwa kawaida tumbo la binadamu hutengeneza lita 2 za tindikali (Hydrochloric acid) kwa siku

10. Imegundulika kwamba kucheka ni dawa nzuri ya maumivu (painkiller)




11. Mtu hutumia misuli 200 kupiga hatua moja anapotembea. Hii inajumuisha misuli ya miguu pamoja na mikono.


12. watoto wana mifupa mingi kuliko watu wazima. Watoto wana mifupa 300 wakati watu wazima wana mifupa 206. Hii inatokana na kwamba baadhi ya mifupa ya watoto huungana pamoja wakati anapoelekea utu uzima.

13. Binadamu anapofikisha miaka 18 chembe hai (seli) zake za ubongo huacha kukua na badala yake huanza kufa. 

No comments:

Post a Comment